VIONGOZI WA PAROKIA

VIONGOZI WA PAROKIA

Sunday 29 March 2015

JUKWAA LA VIJANA


Hii ni sehemu au ulingo (platform) ulio huru wa vijana hasa wa Ubungo Msewe kukaa chini na kuzungumzia masuala ambayo yataleta chachu kuwaendeleza kiuchumi,kijamii na kiroho katika mahali wanamoishi.
Tumezoea sana vijana wengi wanakuwa wakitegemea ajira pekee kama sehem ya kujipatia kipato kumbe wanasahau wanaweza kujiendeleza wenyewe kwa kufanya shughuli za kijasiriamali.
Hivyo kila kijana katika parokia ya Ubungo Msewe ana wajibu wa kuwa sehem ya hili jukwaa na kuleta mawazo yake chanya kwa maendeleo ya vijana wote.
Jukwaa hili litafanyika kila jumapili ya mwisho wa mwezi na litakuwa likisimamiwa na Spika Frank Kondo na Msaidiz wake Albert Msamia huku likiwezeshwa na mlezi kaka Charles ........
Uongozi wa vijana parokia utajitahidi kufanya jukwaa hili kila Juma Lpili ya mwisho wa mwezi vijana wote mnaombwa msikose.
Imeandikwa na Spika wa jukwaa Frank Kondo
Akisaidiana na Albert Msamila naibu Spikaa

No comments:

Post a Comment